DICHIARAZIONE DI FIUGGI - DONNE IN MUSICA

Roma, settembre 2000

Albanese Arabo - Cinese - Croato - Inglese - Finlandese - Francese - Tedesco - Greco - Ebraico
Italiano - Giapponese - Kinswahili - Persiano - Polacco - Portoghese - Rumeno - Russo - Serbo
Spagnolo - Svedese - Tagalog - Ukraino

AZIMIO LA WANAWAKE KATIKA MUZIKI – ROMA, SEPTEMBA 2000
Mwishoni mwa kongamano la kwanza la kimataifa “Donne in Musica Gli Incontri al Borg, Fiuggi” mwaka wa 1996, wanamuziki wa kike kutoka inchi ishirini na sita “26” ukijumuisha watungaji, wasanii, viongozi, wasomi wa muziki na watayarishaji, waliithinisha stakabathi ijulikanayo “Azimio La Fiuggi 1996”.

Azimio hili ambalo limesambazwa kote duniani kwa wanawake katika mashirika ya muziki na usomi, huangazia yale amboyo ni malengo ya musingi kulingana na wanamuziki wa kike.

Munamo mwaka wa 1999, azimio hili lilifanywa marekebisho na kukubaliwa kwa umoja munamo September 2000. Hii ilifatiwa na kukubaliwa na kamati ya wakfu wa utunzaji katika Roma. Stakabadhi hii, inajumuisha yafuatayo:

Kila inchi inakaribishwa kuendeleza uundaji wa mashirika ya kutoa stakabadhi na habari kuhusu wanawake watungaji na mipaka yao ya kitaifa. Mashirika haya lazima yaweze kutoa na kupata habari kuhusu wanamuziki wakike hasa katika usambazaji na utoaji wa muziki. Tamasha za muziki wa kisasa na wakale, tamasha za kuhusisha wanawake pekee, uwezekano wa kufadhiliwa na kudhaminiwa kwa masomo ya wanawake wapewe kipao mbele katika utoaji na uenezaji wa muziki ili kuongoza ujuzi katika muziki. Wanawake wachukue nafasi ya kwanza katika uandaaji wa muziki katika inchi zao na kuendeleza uhusiano kati ya watungaji na wasanii. Mashirika haya yaweza kuunganishwa kupitia mutandao “WWW”. Utungaji wa sheria katika inchi nyingi huwapa wanawake nafasi sawa na haki kimawazo na lazima pia wapewe nafasi sawa katika nyanja zote za kujiendeleza. Katika utendaji, hili huwa sivio. Wanawake katika makundi ya muziki lazima waone kama maisha ya jamii yanaenda sambamba na sheria zilizoko. Katika inchi nyingi wanawake hawajawakilishwa ipasavyo katika tahasisi hizi. Lazima tuhakikishe kua, wanawake wanashirikishwa kwenye majopo na kamati na sehemu zingine ambapo talanta zao zahitajika.

Wanasiasa wanawake lazima wafahamu tofauti zilizoko baina ya uundaji sheria na utekelezaji na wapiganie kwa niaba ya wanamuziki wa kike kupata ufadhili. Habari kuhusu wanamuziki wakike lazima zipewe kwa walimu wa muziki wake kwa waume. Majukumu yanayotekelezwa na wanawake katika muziki lazima yajumuishwe kwa ratiba ya masomo katika shule, viuo na viuo vikuu.

Wazazi nao wasaidie watoto wao waschana kwa wavulana kutambua na kuendeleza vipawa viao katika muziki. Hii itasaidia kujivunia nakuendeleza itikadi na utamaduni wao. Wanamuziki wa kike wanahimizwa kusoma, kujipa mwoyo na watumie sitakabadhi ya shirika la umoja wamataifa linalo husika na maswala ya elimu, sayanzi na utamaduni “UNESCO” kuhusu haki za musanii na sitakabadhi ya mwisho kutoka kwa kongamano la serikali kuhusu sera za kitamaduni ulio fanywa Stockoholm mwak wa 1998. Juhudi za wanawake katika utamaduni na maendeleo, yafaa yaangaziwe na washirikishwa kwenye uandaji wa sera za kitamaduni katika nyanja zote. Hatuna budi kuhifadhi, kuendeleza na kutetea talanta za usanii wa wanawake katika jamii. Hii ndio njia pekee ya kushinda zana za ubaguzi wa utamaduni zilizo buniwa na wanaume. Jukumu letu katika kuangazia maswala bayana na yasio bayana hayawezi kupuuzwa kwasababu hayahusu tu watu au utamaduni, bali pia ubinadamu kwa ujumula.